Connection

Services

Computer Maintanance

Computer Supply

Laptop Repair

Networking Installation



Learn more

Wednesday, 14 August 2013

Filled Under:

MICHEZO

Share

Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez anaonekana kuwa amebadili mawazo yake na kuamua kubaki na klabu hiyo .
Kwa mujibu wa taarifa iliyonukuliwa toka kwa mwandishi wa habari aliye karibu na Suarez Martin Chaquero Suarez amemhakikishia mwandishi huyo kuwa ameamua kubaki ndani ya klabu hiyo ambapo ameeleza sababu yake kubwa ya kubadili mawazo ni imani kubwa na upendo toka kwa mashabiki wa klabu hiyo kuelekea kwake katika kipindi chote hiki.
Suarez amesema kuwa mashabiki wa The Kops wamemuonyesha iamni kubwa ambayo hana njia nyingine ya kuilipa zaidi ya kubaki ndani ya klabu hiyo.
Kwa muda mrefu katika kipindi hiki ambapo dirisha la usajili liko wazi Luis Suarez amekuwa akielezea azma yake ya kutaka kuondoka ndani ya Liverpool sababu yake kubwa ikiwa kutaka kucheza Ligi ya Mabingwa barani ulaya .
Klabu ya Arsenal ilipeleka ofa mbili za kumnunua mshambuliaji huyo lakini Liverpool ilizikataa ofa zote .
Kocha wa Liverpool Brendan Rogers mwanzoni mwa wiki iliyopita alimpa Suarez adhabu ya kufanya mazoezi mwenyewe kwa kuikosea heshima klabi hiyo baada ya kufanya mazungumzo na waandishi wa habari na kuwaambia kuwa Liverpool ilimuahidi kuwa ingemruhusu aondoke .
Suarez-Rodgers
Kwa mujibu wa mwandishi huyo Martin Chaquero Suarez amesema kuwa kuna uwezekano way yeye kuongeza mkataba ambao utamfanya aendelee kuwa na Liverpool kwa muda mrefu zaidi.
Hata hivyo mshambuliaji huyo bado amegoma kuwaomba wachezaji wenzie msamaha kama alivyoamriwa na kocha wake kwa kitendo cha kuwakosea heshima kwa kuzungumza na vyombo vya habari.

0 comments:

Post a Comment

2014 © Movieism
RealMag theme by Templateism