Picha hii ilipigwa Sudan wakati wa njaa kali miaka kadhaa iliyopita. Huyo mtoto alikuwa anatambaa kuelekea walipo watoa misaada wa mashirika ya UN, na akawa anazidiwa kutokana na njaa kali, huku huyo tai akiwa standby anamsubiria afe ili aanze kufaidi mzoga. Mpiga picha wa picha hiyo inasemekana alikuwa ni Mwingereza, ambaye baada ya kukishuhudia hicho alichokiona hapo, na kupiga picha hiyo, alijinyonga kutokana na msongo wa mawazo.
mpiga picha alimuacha na kuondoka bila kumsaidia huyo mtoto, baadaye
ikajulikana kuwa huyo mtoto alikufa na kuliwa na huyo tai. habari hii
ilipoenea na mpiga picha alishutumiwa sana na wanaharakati na hata
mchumba wake waliyetarajia kufunga naye ndoa alimkataa kwa kusema hataki
kufunga ndoa na mtu katili kama huyo! hayo mashutumu toka kwa watu
mbalimbali yalipomzidi alijuiua kwa kujinyonga! mpiga picha huyo anaitwa kevin carter
huyu hapa chini
Huyu aliamua kuoga kwa mkojo wa ngamia
0 comments:
Post a Comment