Connection

Services

Computer Maintanance

Computer Supply

Laptop Repair

Networking Installation



Learn more

Wednesday, 25 September 2013

Filled Under:

MICHEZO

Share

LEO OLD TRAFFORD: NI MAN UNITED v LIVERPOOL!


>>FOWLER: ‘NI NAFASI YA MWISHO KWA SUAREZ!’
>>KWA MOYES NA MAN UNITED, NI USHINDI AU WASHABIKI ‘WATAASI!’



EVRA_N_SUAREZLEO USIKU Old Trafford ni mtanange babu kubwa kati ya Mahasimu wakubwa Kihistoria wa Soka huko England, Manchester United na Liverpool, wanaokutana kwenye Raundi ya Tatu ya Capital One Cup huku Mechi hiyo ikigubikwa na mvuto wa aina mbili.
Mvuto wa kwanza ni nini kitatokea leo kwa Mabingwa wa England, Manchester United, ambao chini ya Meneja mpya David Moyes, Juzi Jumapili walibamizwa Bao 4-1 na Mahasimu wao wa Jiji la Manchester, Man City, Uwanja wa Etihad kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
Mvuto wa pili ni Luis Suarez, Straika ‘Macheche’ wa Liverpool ambae leo hii ndio itakuwa Mechi yake ya kwanza tu baada ya kumaliza Kifungo cha Mechi 10 alichopewa tangu Mwezi Aprili kwa kumng’ata Meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic wakati wa Mechi ya Liverpool na Chelsea.
+++++++++++++++++++++++++++
CAPITAL ONE CUP
RAUNDI YA TATU
RATIBA
Jumatano Septemba 25
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Birmingham v Swansea
Manchester United v Liverpool
Newcastle v Leeds
Tranmere v Stoke
[Saa 4 Usiku]
West Brom v Arsenal
+++++++++++++++++++++++++++
David Moyes: Ukicheza na Liverpool ni upinzani mkubwa!!
Hapo Jana, David Moyes, wakati wa Mahojiano na Wanahabari, alisema: “Ukiwa Meneja kwa muda mrefu kama nlivyokuwa mimi, Siku zote utapata mistuko. Nishapata mingi. Sina wasiwasi itakuwepo mingine baadae. Hivi ndivyo Soka lilivyo. Huwezi kukaa muda mrefu unafikiria hayo. Yamepita hayo, siwezi kufanya lolote kuhusu hayo, tunasonga mbele. Tunaangalia Gemu ijayo na kujaribu kushinda. Nina motisha kwa kila Gemu.”
Akiongelea Mechi hiyo ya Capital One Cup dhidi ya Liverpool, Moyes amesema: “Ni Gemu muhimu kwetu. Tunataka kujaribu kufanya vyema katika Vikombe vyote. Siku zote ni Gemu kubwa ukicheza kwenye Vikombe. Ukicheza na Liverpool ni upinzani mkubwa. Inaweza ikachukuliwa ni Gemu kubwa kwa sasa lakini mwishoni ni Mechi kama nyingine tu.”
Kuhusu ile desturi ya kuchezesha Chipukizi kwenye Mashindano haya ya Capital One Cup, Moyes alieleza: “Kombe hili Siku zote limekuwa ni njia ya kujaribu na kuwapa nafasi Vijana. Lakini inategemea Droo yenyewe na wakati mwingine unaweza kufanya hivyo. Lakini hii ni Mechi kubwa iliyotoka kwenye Droo hiyo.”
Robbie Fowler: Luis Suarez nafasi ya mwisho kwake Liverpool!!
SUAREZ_n_IVANOVICNae Mchezaji wa zamani wa Liverpool, Robbie Fowler, amesema hii ni nafasi ya mwisho kwa Luis Suarez ambae pia ana wajibu wa kulipa fadhila kwa Klabu hiyo.
Fowler amesema: “Nadhani Suarez ataanza katika Mechi hii kwa sababu mbili: kwanza anahitaji Mechi na bila ya kuwepo kwa Philippe Coutinho alieumia ipo nafasi kwake. Ukweli ni kuwa kama Liverpool haitamaliza katika 4 bora Msimu huu, Suarez ataondoka.”
Alipohojiwa kama hii ni nafasi ya mwisho kwa Suarez kujirekebisha kwa tabia zake za utovu wa nidhamu, Fowler alijibu: “Bila shaka. Amewaangusha Watu wengi sana, ikiwa pamoja na yeye!”
Fowler, ambae alifunga Bao 183 katika Mechi 369 kwa Liverpool, amesema: "Klabu ilikuwa upande wake na kumsapoti, pia Masapota, na hii ni kwa sababu ni Mchezaji mzuri mno. Ndio alisinikiza kuhama lakini bado yupo Liverpool. Sidhani kama atapata nafasi nyingi akileta upumbavu wake Uwanjani!”
Suarez alihamia Liverpool kutoka Ajax Januari 2011 lakini tangu wakati huo amekumbwa na utata mkubwa Uwanjani na kufungiwa mara kadhaa na kutwangwa Faini.
+++++++++++++++++++++++++++++++
PATA MATUKIO YA UTATA YA SUAREZ KATIKA ULIMWENGU WA SOKA:
Novemba 2007
Akiwa Nahodha wa Ajax alifungiwa na Klabu yake baada ya kupigana na mwenzake Albert Luque wakati wa Haftaimu kwenye Mechi.
Julai 2010
Afrika na Dunia nzima itamkumbuka Suarez, ambae ni Mchezaji wa Uruguay, kwa kuikatili Ghana huko Afrika Kusini kwenye mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Dunia alipoushika mpira kwa makusudi kwenye mstari wa goli dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza na kuwanyima Ghana goli la wazi la ushindi.
Kwa kitendo hicho, Suarez aliwashwa Kadi Nyekundu na Ghana kupewa penati lakini Asamoah Gyan, ambae aliwahi kuwa Ligi Kuu England na Timu ya Sunderland, alikosa kufunga penati hiyo.
Novemba 2010
Alipata Kifungo cha Mechi 7 akiwa huko Uholanzi  na Klabu ya Ajax baada ya kumng’ata meno Mchezaji wa PSV Eindhoven Otman Bakkal kwenye mechi ya Ligi huko Uholanzi.
Octoba 2011
Wakicheza na Everton, alivunga amechezewa faulo na Jack Rodwell na kujidondosha na Rodwell akapewa Kadi Nyekundu.
Octoba 2011
Suárez alimkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kufungiwa Mechi 7 na kupigwa Faini Pauni 40,000.
Decemba 2011
Akiwa kwenye mashitaka ya kumkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kabla hajahukumiwa alionekana kutoa ishara ya matusi kwa Mashabiki wa Fulham kitendo ambacho kilimpa Kifungo cha Mechi 1.
Februari 2012
Man United na Liverpool walikutana tena Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu tukio la Suarez kumkashifu Kibaguzi Evra na Suarez, bila kutarajiwa, aligoma kumpa mkono Evra.
Octoba 2012
Alishangilia Goli lake kwa kujirusha mbele ya Meneja wa Everton, David Moyes, ambae kabla ya Mechi hiyo na Liverpool alitamka Wachezaji wadanganyifu kama Suarez wnaohadaa Marefa wanafanya Mashabiki waikatae Soka ya England.
Januari 2013
Alipoza mpira kwa mkono na kufunga Bao la ushindi kwa Liverpool kwenye Mechi ya Raundi ya 3 ya FA CUP dhidi ya Timu ya Daraja la chini Mansfield.
Machi 2013
Akiichezea Nchi yake Uruguay kwenye Mechi ya Mchujo ya kuwania kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014, Suarez alionekana kumtandika ngumi Beki wa Chile Gonzalo Jara bila Refa kuona.
FIFA walichunguza tukio hili na kutochukua hatua yeyote.
+++++++++++++++++++++++++++++++
Robbie Fowler amemtaka Suarez kuonyesha uaminifu wake kwa Liverpool pale aliposema : “Wapo Wachezaji wanaofanya vitu vya kipumbavu na kijinga, si sawa lakini unategemea uaminifu toka kwao. Usiruhusu Watu wakunyooshee kidole nenda Uwanjani fanya Vitu sahihi na uwe Mchezaji mwenye Kipaji ambacho tunajua unacho! Sasa tuanze kuongea kuhusu Suarez Mchezaji Bora na si Mchezaji anaefanya upumbavu Uwanjani!”

TATHMINI>>CAPITAL ONE CUP-Raundi ya Tatu: Man United v Liverpool
UWANJA: Old Trafford
SIKU: Jumatano Septemba 25 SAA: 3 Dak 45 Usiku

CAPITAL_ONE_CUP-LOGO28AUG13Hali za Wachezaji
STAA wa Manchester United Robin van Persie huenda asicheze Mechi hii kwani anasumbuliwa na Nyonga iliyomfanya pia aikose Mechi ya Jumapili iliyopita na Man City.
Pia, Mabeki wa Man United, Rafael na Phil Jones, wapo kwenye hatihati lakini upo uwezekano wa Mawinga Nani na Wilfried Zaha kucheza.
Fowadi wa Liverpool Luis Suarez yupo huru kucheza baada ya kumaliza Kifungo cha Mechi 10.
Liverpool huenda ikamkosa Beki Daniel Agger mwenye tatizo la mbavu lakini Glen Johnson, Philippe Coutinho na Joe Allen ni majeruhi.
Tathmini
Kawaida Mechi za Kombe la Ligi, ndio hili Capital One Cup, Klabu huchezesha Wachezaji Chipukizi na wale ambao hawana Namba za kudumu kwenye Kikosi cha Kwanza lakini hii ni Bigi Gemu, Manchester United v Liverpool, na ndio Mechi ya kwanza tu tokea Man United wafungwe na Mahasimu wao wengine Man City na pia hii ni nafasi ya kwanza kwa Luis Suarez kuichezea Liverpool tokea Aprili baada ya kuwa Kifungoni, hivyo tegemea Wachezaji Mastaa na ‘fulu nondo’ toka kila Timu.
Uso kwa Uso
-Kwenye Kombe la Ligi, Manchester United na Liverpool zimekutana mara 4 na Liverpool kushinda Fainali za 1983 na 2003 na pia Mechi ya Raundi ya Nne Mwaka 1985 huko Anfield huku Man United wakishinda Mechi ya Raundi ya Tatu Uwanjani Old Trafford Mawaka 1991.
-Uwanjani Old Trafford, Man United wameishinda Liverpool mara zote 5 katika Mechi zote 5 zilizochezwa mwisho Uwanjani Old Trafford.
-Mara ya mwisho kwa Man United kufungwa na Liverpool Old Trafford ni Machi 2009 walipofungwa Bao 4-1 kwenye Mechi ya Ligi.
REKODI: USO KWA USO
MAN UNITED USHINDI
SARE
LIVERPOOL USHINDI
LIGI
63
44
54
FA CUP
9
4
4
LIGI CUP
1
0
3
NYINGINE
1
3
2
JUMLA
74
51
63

0 comments:

Post a Comment

2014 © Movieism
RealMag theme by Templateism