Connection

Services

Computer Maintanance

Computer Supply

Laptop Repair

Networking Installation



Learn more

Sunday, 13 October 2013

Filled Under:

NEWS

Share
KISA CHA KUPIGWA RISASI MWANDISHI WA HABARI WA ITV NA RADIO ONE, UFOO SARO NA MAMA YAKE MZAZI KUFARIKI DUNIA PAPO HAPO HIKI HAPA


 

Taarifa za mwanzo za kusikitisha ambazo tumezipata hivi punde zinasema mtu mmoja anayedhaniwa kuwa mume au mchumba wa mwandishi wa habari wa ITV na Radio One Ufoo Saro amefanya mauaji ya kutisha na yeye mwenyewe kujiua.
Akizungumza na radio one kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni kamanda Wambura amesema tukio hilo limetokea majira ya alfajiri ya leo.
Kamanda wambura ameongeza kuwa mwanaume huyo anafanya kazi Umoja wa Mataifa (UN) huko Sudani ila bado haijafahamika kwamba anafanyia kitengo gani (japo kwa habari za mtaani zinasema mtu huyo ni mwanajeshi ila bado hazijathibitishwa)


Kamanda Wambura anasema inasemekana kulikua kuna ugomvi kati ya wawili hao ambapo walishindwa kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo Saro (mama mkwe) na ndipo mwanaume huyo alipomshutumu mama mkwe wake kwamba anamtetea mwanae ndipo alipotoa bastola na kumpiga mama yake na Ufoo Saro Risasi ya kichwa na kumuua papo hapo na kisha akampiga Ufoo Saro risasi ya mbili moja ya tumboni na ingine ya mguuni na kudhani kwamba amemuua kumbe amemjeruhi tu kisha kujipiga mwenyewe risasi ya kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.
TAARIFA ZAIDI NA PICHA ZA TUKIO ZITAKUJA PUNDE HAPA HAPA  MTANDAO WA UHAKIKA 





0 comments:

Post a Comment

2014 © Movieism
RealMag theme by Templateism