

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)
linasikitika kutoa taarifa kuwa, kumetokea tatizo la moto kwenye Kituo
cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha 33kV Ubungo jijini Dar es Salaam
majira ya Saa 9:30 alfajiri usiku wa kuamkia Agosti 22, 2013 na moto huo
ulidhibitiwa kwa ushirikiano wa vikosi vya zimamoto vya Jiji vya Knight
Support na Security Group.
Vifaa
vilivyoharibiwa na moto huo ni pamoja na waya mkubwa za umeme “Power
Cables”, Control Cables na T5 Breaker. Mafundi wa Shirika wanaendelea na
matengenezo na wameshafanikiwa kurudisha umeme kwa baadhi ya maeneo
yaliyoathirika kutokea kwenye vituo vingine vya jirani. Hata hivyo kazi
hiyo inakadiriwa kukamilika kati ya wiki moja na nusu na wiki mbili ili
kurejesha umeme kwenye hali ya kawaida.
Maeneo
yanayoathirika moja kwa moja ni Sinza, Tandale, Shekilango, Magomeni,
Ubungo, Mlimani City, TCRA, Ubungo Plaza, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Chuo cha Ardhi, Makongo, Changanyikeni, Mabibo External, Mburahati,
Manzese, Tabata, maeneo yote ya Barabara ya Mandela Kimara, Mbezi,
Kibamba na maeneo yote ya jirani.
Uongozi wa Shirika unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na: OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.
0 comments:
Post a Comment