SHAKHTAR DONETSK v MAN UNITED, NI HEKAHEKA!!
>>KOCHA MIRCEA LUCESCU: ‘MOYES ANAATHIRIKA KWA KUBADILISHA TIMU SANA!’

Hii ni Mechi ya pili kwa kila Timu
kwenye Kundi A na Shakhtar Donetsk ilianza vyema kwa ushindi wa Ugenini
wa Bao 2-0 dhidi ya Real Sociedad na Man United kuichapa Bayer
Leverkusen Bao 4-2 Uwanjani Old Trafford.
Wakati kwa David Moyes hii ni mara ya
pili kuongoza Timu kwenye UCL, na ikiwa ni Mechi ya pili tu kwake na Man
United, Lucescu anaongoza Kikosi kwa mara ya 109 kwenye Mechi za UCL na
pia alikuwepo kama Meneja kwenye Timu ya Inter Milan ya Mwaka 1999
iliyotolewa na Man United kwenye UCL na Man United kutinga Fainali na
kuichakaza Bayern Munich na kuwa Bingwa.
Siku 3 baada ya Mechi hiyo ya Robo
Fainali huko San Siro ambayo Inter Mian waliongoza kwa Bao 1 na Man
United kurudisha na hatimae kutinga Fainali, Mircea Lucescu alijiuzulu
Umeneja Inter Milan.
Lucescu, Kocha Mkongwe mwenye Miaka 68,
ameeleza: “Kila Kocha mpya anakuja na falsafa yake na inachukua muda.
Lakini tumechunguza Gemu za United na tumeona kila Mechi anabadili
Wachezaji labda wanne au watano. Ubadilishaji huu unasababisha Wachezaji
kupoteana.Tumeona Klabu nyingine kubwa huko England Chelsea, Liverpool
na Arsenal hawabadili sana na pengine hii ndio sababu hawafanyi vizuri.”
TATHMINI YA MECHI:
>>DONBASS ARENA, DONETSK, UKRAINE JUMATANO SAA 03:34 USIKU
Man United wanaingia kwenye Mechi hii
wakitokea kwenye Wiki ngumu ambayo walifungwa 4-1 na Man City kwenye
Ligi, kuifunga Liverpool 1-0 kwenye Capital One Cup na kufungwa 2-1 na
West Brom kwenye Ligi.
Shakhtar Donetsk wao Jumamosi iliyopita
walitoka nyuma 2-0 na kutoka Sare 2-2 na Wapinzani wao wakubwa wa Mjini
Donetsk, Metallurg Donetsk, kwenye Mechi ya Ligi Kuu ya Ukraine.
Man United na Shakhtar Donetsk
hazijawahi kukutana lakini Man United wameshacheza na Klabu ya Ukraine
Dynamo Kiev mara 4 na kushinda mara 3 na sare 1.
Shakhtar imesheheni Wachezaji toka
Brazil na Kiungo Alex Teixeira ndie Nyota ambae pia ndie aliefunga Bao
zote 2 walipoitwanga Real Sociedad Bao 2-0 kwenye Mechi ya kwanza ya
Kundi hili.
VIKOSI:
MANCHESTER UNITED:
MENEJA: David Moyes
MAKIPA: 1. David De Gea, 13, Anders Lindegaard, 50. Sam Johnstone;
MABEKI: 2. Rafael da
Silva, 3. Patrice Evra, 4. Phil Jones, 6. Jonny Evans, 12. Chris
Smalling, 15. Nemanja Vidic, 28. Alexander Büttner, 39. Tom Thorpe;
VIUNGO: 8. Anderson,
11. Ryan Giggs, 16. Michael Carrick, 17. Nani, 18. Ashley Young, 23. Tom
Cleverley, 25. Antonio Valencia, 26. Shinji Kagawa, 31. Marouane
Fellaini,
MASTRAIKA: 10. Wayne Rooney, 14. Javier Hernandez, 19. Danny Welbeck, 20. Robin van Persie,
SHAKHTAR DONETSK:
MENEJA: Mircea Lucescu
MAKIPA: 30. Andriy Pyatov, 32. Anton Kanibolotskiy, 35. Mykyta Kriukov;
MABEKI: 4. Olexandr
Volovyk, 5. Olexandr Kucher, 13. Vyacheslav Shevchuk, 27. Dmytro
Chygrynskiy, 38. Serhiy Kryvtsov, 44. Yaroslav Rakitskiy;
VIUNGO: 3. Tomáš
Hübschman, 6. Taras Stepanenko, 8. Fred, 10. Bernard, 14. Vasyl Kobin,
17. Fernando, 20. Douglas Costa, 24. Dmytro Grechyshkin, 29. Alex
Teixeira, 33. Darijo Srna, 77. Ilsinho;
MASTRAIKA: 9. Luiz Adriano, 11. Eduardo, 19. Facundo Ferreyra, 28. Taison
REFA: Pavel Kralovec [Czech Republic]
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumatano 2 Oktoba 2013
[Saa 1 Usiku]
PFC CSKA Moskva v FC Viktoria Plzeň
[Zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku]
FC Shakhtar Donetsk v Manchester United FC
Bayer 04 Leverkusen v Real Sociedad de Fútbol
Juventus v Galatasaray A.Ş.
Real Madrid CF FC København
Paris Saint-Germain v SL Benfica
RSC Anderlecht v Olympiacos FC
Manchester City FC v FC Bayern München
0 comments:
Post a Comment