Connection

Services

Computer Maintanance

Computer Supply

Laptop Repair

Networking Installation



Learn more

Monday, 16 September 2013

Filled Under:

MICHEZO

Share
KATIKA KILE KILICHOZUNGUMZWA KUWA MAN UTD IMEBEBWA KWA KUPEWA PENATI MOYES KUMWONYA YOUNG KUHUSU KUJIANGUSHA


Meneja wa Manchester United David Moyes amewaonya Wachezaji wake kuwa hatavumilia vitendo vya kujiangusha makusudi ili kuhadaa Marefaa kufuatia Ashley Young kupewa Kadi ya Njano kwenye Mechi ya ya Ligi Kuu England waliyoifunga Crystal Palace Bao 2-0 
Katika Mechi hiyo Young alianguka ndani ya boksi baada ya kupambana na Kagisho Dikgacoi katika Kipindi cha Kwanza lakini marudio kwenye TV yalionyesha ni Young ndie aliemgonga Mchezaji huyo kutoka Afrika Kusini.
Tukio hilo ndilo lilimpa Kadi Young lakini baadae kwenye Kipindi hichi hicho Young aliangushwa na Dikgacoi na Refa Jon Moss akaipa Man United Penati na kumpa Kadi Nyekundu Dikgacoi kwa tukio hilo.
Na Moyes amesema: "Sitaki Wachezaji wangu wajiangushe kuhadaa Marefa. Tukio la kwanza Dikgacoi alinyoosha Mguu lakini Ashley aliusogeza Mguu wake ugongane."
Hata hivyo Moyes aliunga mkono uamuzi wa kutoa Penati kwa tukio la pili kati ya Young na Dikgacoi lakini amesema hapendezewi na Sheria ya kutoa Penati na Kadi Nyekundu kwa pamoja.
Nae Meneja wa Crystal Palace, Ian Holloway, ambae Jana alikuwa akianza kutumikia Kifungo chake cha Mechi mbili alichopewa baada ya kubatukia Marefa katika Mechi yao ya kwanza ya Ligi waliyocheza na Tottenham.

0 comments:

Post a Comment

2014 © Movieism
RealMag theme by Templateism